Polisi wachunguza tukio la dada wa Polepole

By Mwandishi Wetu , Nipashe
Published at 01:06 PM Jul 18 2025
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro.

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limethibitisha kupokea taarifa za kutekwa na kurejeshwa kwa mwanamke aliyejitambulika kwa jina la Christina Hezroni Polepole Kinyangazi, mwenye umri wa miaka 52, mkazi wa Bahari Beach, mtaa wa Katumba, Kinondoni.