Wodi ya wazazi Hosptali Rufani Temeke, wakumbukwa

By Jumanne Juma , Nipashe Jumapili
Published at 04:28 PM Mar 09 2025
Mariagoreth Mkenda (kushoto), akimpatia msaada mmoja wa
mzazi, Zamoyoni Rashid, aliyejifungua katika Hospital ya Rufaa ya Mkoa
wa Temeke
Picha: Jumanne Juma
Mariagoreth Mkenda (kushoto), akimpatia msaada mmoja wa mzazi, Zamoyoni Rashid, aliyejifungua katika Hospital ya Rufaa ya Mkoa wa Temeke

WODI ya wazazi katika Hospitali ya Rufani ya Mkoa wa Temeke, Dar es Salaam, wamepokea msaada wa vitu mbalimbali, kwa wodi hiyo, pia kwa wauguzi na watoa huduma.

Akizungumza kwa niaba wafanyakazi wenzake, Ofisa Rasilimali Watu wa kampuni hiyo, Mariagoreth  Mkenda, amesema msaada waliotoa ni kwa sababu ya kutambua thamani ya mama.

Pia, alisema wanatambua umuhimu wa sekta nzima ya afya kwa ujumla katika kipindi hiki  cha siku ya wanawake dunia na kuwaomba wanawake wote kuwa na imani na wauguzi wanaowapatia matibabu mara wanapofika hospitalini hapo kupata matibabu,

Aye mmoja wa wazazi aliyejifungua katika hospitali hiyo, Zamoyoni Rashid, amewashukuru wanawake wa kampuni hiyo kwa kuwajali wanawake wenzao kwa kujitole msaada utakaowasaidia kutokana na baadhi yao hupungukiwa na vitu kutokana kosa pesa za kununu na kutokana na msaada huo walioupata kutoka Kisima Water utawasaidia sana,

Naye Kaimu Muuguzi Mkuu wa Hospitali hiyo, Beatrice Temba, amesema kwa niaba ya uongozi wa hospital hiyo wanatoa shukrani zao kwa wanawake wa Kampuni ya  Kisima kwa kujitolea msaada wao kwa wanawake wenzao wanapata huduma hospitalini hapo

Amesema kuwa wanawake lazima tushikane mkono ili tuwe wazazi bora katika jamii.