Ushauri wa INEC kuelekea Uchaguzi Mkuu uzingatiwe
WAKATI nchi yetu ikielekea kwenye Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba, mwaka huu, Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imewataka watendaji wa uchaguzi huo kufanya vikao na viongozi wa vyama vya siasa ili kujadili masuala mbalimbali yakiwamo ya uteuzi wa wagombea.