Kunje Mwiru: Amani ndio msingi wa maendeleo

By Imani Nathaniel , Nipashe Jumapili
Published at 06:35 PM May 04 2025
Mgombea Urais kupitia Chama cha Allience For Africa Farmers Party(AAFP) , Kunje Ngombale Mwiru akizungumza na waandishi.
PICHA: IMANI NATHANIEL
Mgombea Urais kupitia Chama cha Allience For Africa Farmers Party(AAFP) , Kunje Ngombale Mwiru akizungumza na waandishi.

Mgombea Urais kupitia Chama cha Allience For Africa Farmers Party(AAFP) , Kunje Ngombale Mwiru' amewashukuru wanachama na wajumbe wa chama hicho kwa kumchagua kuwa mgombea wa Urais kupitia chama hicho katika uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika mwaka huu huku akitaka amani itawale.

Shukrani hizo amezitoa leo Mei 4, 2025 wakati akizungumza na waandishi wa habari  mbali na kuwashukuru wajumbe na wanachama ameishukuru pia Ofisi ya  Msajili wa Vyama vya Siasa,  kwa kusimamia zoezi la kupitisha mgombea. Katika mkutano mkuu maalum wa chama uliofanyika April 29, 2025 Temeke Jijini Dar es Salaam. 

mwiru.jpeg 122.03 KB
Aidha amesisitiza  kuwa Serikali yake itakuwa ya mchakamchaka kwani mabadiliko yatahitaji kufanya kazi usiku na mchana .Asema amani ndio Msingi mkubwa katika maendeleo ya taifa na kuwaomba wanasiasa kuzingatia swala la amani kwani hakuna nchi iliyoimarika kukiwa na vurugu za aina yoyote.