Nchemba azuru Uganda, wateta diplomasia

By Ambrose Wantaigwa , Nipashe Jumapili
Published at 03:48 PM Mar 16 2025
Waziri wa Fedha, Dk. Mwigulu Nchemba, akiwa na Balozi wa Tanzania nchini Uganda, Meja Jenerali Paul Simuli katika ofisi za ubalozi huo
Picha: Mpigapicha Wetu
Waziri wa Fedha, Dk. Mwigulu Nchemba, akiwa na Balozi wa Tanzania nchini Uganda, Meja Jenerali Paul Simuli katika ofisi za ubalozi huo

WAZIRI wa Fedha, Dk. Mwigulu Nchemba ametembelea Ofisi za Ubalozi wa Tanzania, ziizopo Kampala nchini Uganda na kufanya mazungumzo na Balozi wa Tanzania nchini humo, Meja Jenerali Paul Simuli

Nchemba, alifika katika ubalozi huo, baada ya kuhitimisha Mkutano wa 50 wa Benki ya Maendeleo Afrika Mashariki (EADB) na kumpongeza balozi huyo na watumishi wa Ubalozi kwa kazi nzuri wanayofanya.

Katika taarifa iliyotolewa kupitia  ukurasa rasmi wa X wa wizara hiyo, Machi 15, 2025 ilieleza kwamba Nchemba, lisisitiza umuhimu wa kuendelea kuimarisha diplomasia ya uchumi baina ya mataifa hayo mawili.

Alisema wananchi wa pande zote wanapaswa kuzitumia fursa mbalimbali za ukuzaji biashara kwa manufaa ya nchi hizo mbili, ikizingatiwa kuwa Tanzania na Uganda ni nchi rafiki na zina historia kubwa na ya kujivunia.

Katika ziara hiyo, Nchemba aliambatana na Kamishna wa Idara ya Uendelezaji Sekta ya Fedha, Wizara ya Fedha, DktCharles Mwamwaja na maofisa wengine wa serikali.

Tayari Benki ya Maendeleo ya Afrika Mashariki (EADB), imeahidi kuendeleza ushirikiano uliopo kati yake na Tanzania kwa kuendelea kufadhili miradi mbalimbali ya maendeleo nchini.