RC Macha atamani ufaulu kitaifa mkoani mwake

By Marco Maduhu , Nipashe
Published at 03:02 PM Apr 06 2025
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Anamringi Macha, akizungumza kwenye kikao cha Tathimini ya Elimu mkoani humo na kutaka ufaulu mzuri wa wanafunzi
Picha: Marco Maduhu
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Anamringi Macha, akizungumza kwenye kikao cha Tathimini ya Elimu mkoani humo na kutaka ufaulu mzuri wa wanafunzi

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga, Anamringi Macha, amewasisitiza walimu wa shule za msingi na sekondari mkoani humo, kufanya kazi kwa bidii na weledi katika kufundisha wanafunzi shuleni, ili kuinua ufaulu wao na kushika nafasi nzuri kitaifa.

Amesema kwamba muda mrefu mkoa huo hauna matokeo mazuri.

Amebainisha hayo wakati akifungua Kikao Kazi cha  Wadau wa Elimu mkoani humo na kufanya tathimini, kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Shinyanga Butengwa.

Amesema mkoa huo wa muda umekuwa haufanyi vizuri kitaifa katika kufaulisha wanafunzi na kuwataka walimu waongeze bidii katika ufundishaji wao, ili kuongeza ufaulu na hata kushika nafasi nzuri kitaifa.

RC Macha atamani ufaulu kitaifa mkoani mwake
“Ninawasisitiza sana walimu wa shule za msingi na sekondari mkoani hapa, baada ya kikao hiki mwende mkafanye kazi kwa bidii na weledi muwapo shuleni, ili kuboresha na kuinua ufaulu wa wanafunzi,ili mkoa uwe kwenye nafasi nzuri za ufaulu kitaifa, kwani ni muda mrefu sasa hatuna matokeo mazuri,” amesema Macha.
RC Macha atamani ufaulu kitaifa mkoani mwake
Ofisa Elimu Mkoa wa Shinyanga, Samson Hango, akiwasilisha taarifa ya elimu ya mkoa, amesema takribani miaka tisa kuanzia mwaka 2015-2023, mkoa huo umekuwa hauna matokeo mazuri, hivyo kuwataka walimu hao wakajitathmini na kuona namna bora ya kuboresha na kuinua ufaulu wa wanafunzi kuanzia sasa.

Baadhi ya walimu hao, wamemuahidi Mkuu wa Mkoa kwamba, watakwenda kuyafanyia kazi maagizo yake, iili kuhakikisha kwamba mkoa huo, unapiga hatua katika elimu na kuongeza ufaulu wa wanafunzi.