TIMU ya mpira wa miguu ya Dream team FC, imeibuka mshindi wa fainali za Samia Cup, Wilaya ya Kigamboni jijini Dar es Salaam, baada ya kuifunga timu ya Wahenga FC magoli mawili.
Mechi ya fainali ya Samia Cup, ambayo ilifanyika katika viwanja vya Mji Mwema, ilihudhuriwa na mamia ya wananchi sambamba na wadhamini wa mashindano hayo kutoka Dar es Salam.
Mshindi wa fainali hizo ambaye ni Dream Team FC alinyakua kombe, Sh. milioni mbili pamoja na mbuzi watatu, huku mshindi wa pili Wahenga FC, akiondoka na Sh. milionI 1.5 na mbuzi.
Mshindi wa tatu ambaye ni Amazon FC, alikabidhiwa Sh. milioni moja na mbuzi wawili na mshindi wa nne Tandika FC, akiambulia Sh. laki tano na mbuzi mmoja.
Bananga amewataka wadhamini kuendelea kudhamini michezo ambayo unachangia kuibua vipaji kwa vijana.
Mmoja wa wadhamini wa mashindano hayo, Mohamed Haji, amesema wataendelea kudhamini mashindano ya michezo ambayo yanawakutanisha watu mbalimbali na kwamba, baada ya fainali hizo wanatarajia kuanza mashindano ya mpira wa mikono.
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED