JUKWAA la Wahariri (TEF), limetembelea kiwanda cha kuchakata mafuta ya parachichi, Avo Africa kilichopo kijiji cha Mtewele, wilayani Wanging'ombe mkoa wa Njombe.
Akizungumza leo, Aprili 6, 2025, mara baada ya kutembelea kiwanda hicho, Mwenyekiti wa TEF, Deodatus Balile, amesema uwapo wa kiwanda hicho ni mkombozi mkubwa kwa wakulima.
"Naona sasa kuna juhudi kubwa ya watu kuanzishiwa viwanda, kulima mashamba kufanya kila kitu ambacho kinawezekana kuwaondoa katika umasikini, jambo lililotokea hapa kwamba maparachichi yaliyokuwa ‘reject’ leo yananunuliwa kwa Sh. 750 ni mkombozi mkubwa kwa mkulima wa kawaida," amesema Balile.
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED