KIKOSI cha uokoaji ajali ya mgodi katika machimbo ya Nyandolwa wilayani Shinyanga, kimefanikiwa kutoa miili ya watu wawili, huku idadi ya vifo hadi sasa, ikifikia watu wanne na 18 bado wapo chini ya ardhi.
Miili hiyo imetolewa leo, Agosti 17, 2025. Waliofariki ni Marco Ngelela (26) mkazi wa Sengerema na Macha Shabani (43) mkazi wa Misungwi Mwanza.
Chifu Insepkta Mgodi wa Kikundi cha Wachapakazi Fikiri Mziba, akizungumza kuhusu uokoaji, amesema mchakato unakwenda vizuri na kwamba duara namba 106 wameshatoa watu wote na kusalia duara namba 20 na 103.
Aidha, Agost 11, mwaka huu watu 25 walifukiwa mgodini katika machimbo ya Nyandolwa, wilayani Shinyanga na mpaka leo, kati yao watu saba wametolewa na 18 bado wapo chini ya kifusi, huku watatu wakiwa hai na wanne wamefariki.
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED