NLD yaahidi kukomesha rushwa

By Grace Mwakalinga , Nipashe Jumapili
Published at 06:13 PM Aug 31 2025
NLD yaahidi kukomesha rushwa
PICHA: MPIGAPICHA WETU
NLD yaahidi kukomesha rushwa

Mgombea Urais wa Chama cha National League for Democracy( NLD) Doyo Hassan Doyo amesema endapo watanzania watampa ridhaa ya kuongoza nchi, atapambana na rushwa kwenye miradi ya maendeleo na kuweka sheria kali ikiwemo wahusika kunyongwa.

Doyo ametoa kauli hiyo leo wakati akizungumza  na waandishi  wa habari kwenye Ofisi za Chama hicho zilizopo Tandika jijini Dar es Salaam, kuhusu uzinduzi wa kampeni za Chama hicho zinazotarajiwa kufanyika Septemba 4,2025 jijini Tanga.

“Rushwa imekuwa chanzo cha miradi kukwama kwa sababu ya kugawana asilimia. Serikali ya NLD haitavumilia wala kufumbia macho tatizo hili,” amesema  Doyo.

Ameahidi  kuimarisha Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU na mamlaka nyingine  zinazohusika na udhibiti ili kuhakikisha rasilimali za taifa zinawanufaisha Watanzania wote.Amewataka watanzania  kujitokeza kwa wingi kumuunga mkono wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu, akiahidi mageuzi makubwa ya kiuchumi. 

Ameongeza kuwa NLD imesimamisha wagombea 100 wa nafasi ya Ubunge ambao tayari wamekabidhiwa fomu ya kugombea nafasi zao, vilevile wagombea 1000 wa nafasi ya Udiwani.