Haya hapa majina ya walimu wapya walioajiriwa serikalini

By Mwandishi Wetu , Nipashe
Published at 11:57 AM Mar 13 2025
Ajira mpya za walimu.
Picha:Nipashe Digital
Ajira mpya za walimu.

Serikali imewaita kazini walimu wapya 319 wa fani mbalimbali, ambapo halmashauri saba zimenufaika na kuongezewa nguvu kazi hiyo mpya katika sekta ya elimu.

Taarifa ya kuitwa kazini kwa walimu hao ilitolewa jana, Machi 12, 2025, na Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, waombaji wa nafasi za ualimu waliofanya usaili kati ya Septemba 4, 2024, na Februari 24, 2025, wamepangiwa vituo vya kazi kulingana na matokeo yao.

"Katibu wa Sekretarieti ya Ajira anapenda kuwataarifu waombaji kazi wa nafasi mbalimbali waliofanya usaili kuwa matokeo ya waliofaulu yanaweza kupatikana kwenye tangazo hili. Orodha hiyo pia inajumuisha baadhi ya waombaji waliokuwepo kwenye kanzidata (Database) kwa kada mbalimbali, ambao sasa wamepangiwa vituo vya kazi baada ya nafasi kupatikana," inaeleza sehemu ya taarifa hiyo.

Walimu hao wamepangiwa kufanya kazi katika halmashauri zifuatazo:

Halmashauri ya Manispaa ya Songea
Halmashauri ya Manispaa ya Kahama
Halmashauri ya Jiji la Arusha
Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
Halmashauri ya Wilaya ya Iramba
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua

SOMA HAPA: Majina ya walimu wapya walioajiriwa serikalini