KAMISHNA wa Uhifadhi wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA), Musa Kuji, amewataka maofisa na askari wa Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, waliopo Bonde la Ihefu wilayani Mbarali, mkoani Mbeya kuilinda ardhi oevu ya bonde hilo, ambalo ni chanzo kikuu cha Mto Ruaha.
Ametoa agizo hilo kwenye kikao kazi na makamanda wa Jeshi la Uhifadhi wa Vituo vya Doria vya Ikoga, Tagawano, Magda, Ulanga, Kiwale na Ukwaheri, vilivyopo ndani ya hifadhi hiyo ambayo ni ya pili kwa ukubwa nchini.
"Mto Ruaha Mkuu umeendelea kuwa muhimu sana kwa taifa kwa sababu asilimia 60 ya maji yake ni muhimu kwa uhai wa mimeana wanyamapori ndani ya hifadhi yetu ambayo ni muhimu sana,” amesema Kamishna Kuji.
Kamishna Kuji yupo kwenye ziara ya kutembelea hifadhi zote nchini kwa lengo la kufanya mazungumzo na maofisa pamoja na askari, ili kuimarisha ulinzi wa hifadhi hizo, kukuza utalii na kuimarisha ushirikiano na jamii.
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED