DC Ubungo aanisha miradi ya zaidi ya bilioni 8.2

By Imani Nathaniel , Nipashe
Published at 01:39 PM Jun 06 2025
 DC Ubungo aanisha miradi ya zaidi ya bilioni 8.2
Picha:Imani Nathaniel
DC Ubungo aanisha miradi ya zaidi ya bilioni 8.2

Katika hafla ya mapokezi ya Mwenge wa Uhuru katika Wilaya ya Ubungo, Mkuu wa Wilaya hiyo,Albert Msando, ameupokea Mwenge huo na kuwapongeza vijana wanaoukimbiza kwa uzalendo wao pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kinondoni kwa ushirikiano wao katika shughuli hiyo muhimu ya kitaifa.

Akizungumza wakati wa ukaguzi wa Mradi wa Barabara ya Kibwegere–Mpiji Magohe, Msando alieleza kuwa barabara hiyo yenye urefu wa kilomita 1.4 imejengwa kwa gharama ya Shilingi bilioni 2.8 (TZS 2,764,260,330.14) na ni sehemu ya jitihada za Serikali za kuboresha miundombinu ya barabara katika jiji la Dar es Salaam.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni,Saad Mtambule, aliyekabidhi Mwenge huo kwa Wilaya ya Ubungo, alisema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetoa zaidi ya Shilingi trilioni nne kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali katika Wilaya ya Kinondoni, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuwaletea wananchi maendeleo endelevu.

Msando alitaja miradi saba inayotembelewa na Mwenge wa Uhuru katika Wilaya ya Ubungo, yenye jumla ya thamani ya zaidi ya Shilingi bilioni 8.2, kama ifuatavyo:

  1. Mradi wa Barabara ya Kibwegere – Mpiji Magohe
    • Gharama: TZS 2,764,260,330.14
    • Urefu: Km 1.4
    • Eneo: Kata ya Mpiji Magohe

  2. Mradi wa Ujenzi wa Pampu ya Maji (DAWASA)
    • Gharama: TZS 4,256,774,774.45
    • Eneo: Kata ya Kwembe

  3. Mradi wa Nishati Safi (Shule ya Dar es Salaam Girls)
    • Gharama: TZS 23,983,820.00
    • Eneo: Kata ya Kwembe

  4. Mradi wa Ujenzi wa Vyumba 4 vya Madarasa na Matundu 8 ya Vyoo
    • Gharama: TZS 144,188,300.00
    • Shule: Mbezi Inn Secondary
    • Eneo: Kata ya Mbezi

  5. Mradi wa Vijana (Asilimia 10 ya Mapato ya Halmashauri)
    • Gharama: TZS 50,000,000.00
    • Eneo: Kata ya Sinza

  6. Mradi wa Jengo la Upasuaji na Wodi ya Wazazi
    • Gharama: TZS 398,390,352.00
    • Kituo cha Afya: Makurumla
    • Eneo: Kata ya Makurumla

  7. Mradi wa Uboreshaji wa Soko la Mabibo
    • Gharama: TZS 600,000,000.00
    • Eneo: Kata ya Mabibo

Miradi hiyo ni sehemu ya juhudi kubwa za Serikali ya Awamu ya Sita katika kuboresha huduma za kijamii, miundombinu na kuinua ustawi wa wananchi. Kupitia Mwenge wa Uhuru, wananchi wameweza kushuhudia maendeleo yanayoonekana na yanayogusa maisha yao ya kila siku.