Dk.Mpango awakabidhi tuzo PSSSF, ni kwa kuwasapoti TAPSEA

By Mwandishi Wetu , Nipashe
Published at 11:11 PM May 15 2025
Dk.Mpango awakabidhi tuzo PSSSF, ni kwa kuwasapoti TAPSEA
Picha: Mpigapicha Wetu
Dk.Mpango awakabidhi tuzo PSSSF, ni kwa kuwasapoti TAPSEA

Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) umepokea tuzo kutoka kwa Makamu wa Rais,Dk. Philip Mpango, ikiwa ni ishara ya kutambua mchango wa Mfuko huo katika kufanikisha Mkutano Mkuu wa 12 wa Chama cha Waandishi Waendesha Ofisi (TAPSEA), unaoendelea Ngurdoto jijini Arusha.

Akizunhumza baada ya kupokea tuzo hiyo, Meneja Utawala PSSSF Fatma Chondo alisema ni jambo la furaha kwa Mfuko kupata tuzo hiyo na kuahidi kwamba PSSSF itaendelea kufanya kazi kwa karibu na wadau wote ili kuhakikisha kunakuwepo na maendeleo endelevu katika sekta ya hifadhi ya jamii.


Aidha, Katika Mkutano huo PSSSF imeendelea na zoezi la kuchukua alama za vidole kwa wanachama wake wanaoshiriki mkutano huo.


 Zoezi hilo linaendeshwa nchi nzima ambapo watumishi  wa PSSSF wanapita kwenye maeneo ya kazi na kufanya kazi hiyo kwa lengo la kuboresha taarifa na kurahisisha huduma kwa Wanachama.