Serikali yatenga fedha kwa ajili ya Ujenzi wa Daraja la Lumecha

By Mwandishi Wetu , Nipashe
Published at 12:11 PM Jul 11 2024
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu)Jenista Mhagama na Mbunge wa Peramiho akizungumza na wananchi wa Liweta katika Mkutano wa hadhara kuhusu ujenzi wa Daraja la Lumecha unatarajia kuanza hivi karibuni.
Picha: Mpigapicha Wetu
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu)Jenista Mhagama na Mbunge wa Peramiho akizungumza na wananchi wa Liweta katika Mkutano wa hadhara kuhusu ujenzi wa Daraja la Lumecha unatarajia kuanza hivi karibuni.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama ambaye pia ni Mbunge wa Peramiho ameelekeza Wakala wa Barabara za Vijijini na Mjini (TARURA) Halmashauri ya wilaya ya Songea kuhakikisha daraja la Lumecha linajengwa ndani ya kipindi kifupi na kwa ubora.

Waziri ametoa kauli hiyo jana Julai 10,2024 wakati wa ziara yake ya kutembelea Miradi ya maendeleo katika kijiji cha Liweta Halmashauri ya Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma.

“Serikali imetoa kiasi cha Millioni Mia nne kujenga Madaraja na akiba ya fedha itakayobaki itatumika kutengeneza barabara mpaka kijiji cha Liweta ikiwa ni pamoja na kufukia shimo lilopo katika barabara hiyo alisema,” Waziri Mhagama.

kazi ya ujenzi wa barabara ni kazi muhimu naomba wananchi msaidie katika kulinda mradi ili ujenzi ili ukamilike kwa wakati na tufungue njia zitakazochochea uchumia katika kijiji cha Liweta.