Kesi ya rufaa inayowakabili watuhumiwa wanne waliopatikana na hatia ya kubaka kwa kundi na kumuingilia kinyume na maumbile binti mmoja mkazi wa Yombo Dovya, Dar es Salaam, imeahirishwa hadi Juni 9, 2025.
Washtakiwa hao walihukumiwa kifungo cha maisha pamoja na kulipa faini ya Shilingi milioni moja kila mmoja, hukumu iliyotolewa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Dodoma mnamo Septemba 30, 2024.
Jaji Amir Mruma wa Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma, aliyeahirisha kesi hiyo, amesema kuwa itaendelea kusikilizwa tena katika tarehe hiyo iliyopangwa.
Watuhumiwa hao walikutwa na hatia ya kumbaka na kumuingilia kinyume na maumbile binti aliyetambulishwa kwa jina la X, mkazi wa Yombo Dovya, tukio ambalo liliibua taharuki na hasira kwa jamii.
Washtakiwa katika kesi hiyo ni:
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED