Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imetangaza kuanzishwa kwa majimbo mapya nane ya uchaguzi pamoja na kubadilishwa kwa majina ya majimbo mengine 12, ikiwa ni maandalizi ya kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwaka huu.
Akitoa taarifa hiyo leo jijini Dodoma, Mwenyekiti wa Tume hiyo,Jaji wa Mahakama ya Rufani Jacobs Mwambegele, amesema uamuzi huo umezingatia ongezeko la watu, ukubwa wa maeneo ya kiutawala, pamoja na mahitaji ya uwakilishi wa karibu zaidi kati ya wananchi na wawakilishi wao bungeni.
Kwa mujibu wa Jaji Mwambengele, majimbo mapya yaliyoundwa ni kama ifuatavyo:
Aidha, Tume hiyo imesema majina ya majimbo 12 ya uchaguzi yatafanyiwa mabadiliko ili kuendana na mabadiliko ya kiutawala, kijografia na mahitaji ya kitaifa ya utawala bora. Orodha kamili ya majimbo yaliyoathiriwa na mabadiliko ya majina inatarajiwa kutangazwa rasmi katika tangazo la serikali litakalotolewa hivi karibuni.
Tume imewahakikishia Watanzania kuwa mchakato huo umezingatia misingi ya usawa, haki na ushirikishwaji wa wadau mbalimbali, na unalenga kuhakikisha uchaguzi mkuu wa mwaka huu unafanyika kwa uwazi, haki na kwa kuzingatia uwakilishi wa kweli wa wananchi.
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED