Bodi ya kitaaluma ya walimu yaja

By Mwandishi Wetu , Nipashe
Published at 04:37 PM May 12 2025
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof.Adolf Mkenda.
Picha: Bungeni
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof.Adolf Mkenda.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof.Adolf Mkenda amesema kwa mwaka 2025/26, serikali itaanza utekelezaji na uendeshaji wa Bodi ya Kitaalamu ya Walimu ambayo itawezesha usajili na uendelezaji wa walimu wote walioajiriwa katika shule za serikali na zisizo za serikali.

Akiwasilisha leo bungeni makadirio ya mapato na matumizi ya mwaka 2025/26, Prof. Mkenda amesema “Ili  kuhakikisha walimu wanaohitimu katika vyuo vinavyotoa mafunzo ya elimu ya ualimu vinavyotambulika na Serikali wanapata usajili  utakaowawezesha kutambulika ndani na nje ya  nchi pamoja na kuendeleza utaalamu wao.

Aidha, amesema bodi itawezesha usajili na uendelezaji wa walimu  wote walioajiriwa katika shule za serikali na zisizo za Serikali.”