Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof.Adolf Mkenda amesema kwa mwaka 2025/26, itaongeza idadi ya wanafunzi wanaonufaika na mikopo ya elimu ya juu kutoka 245,314 mwaka 2024/25 hadi wanafunzi 252,773.
Akiwasilisha leo bungeni makadirio ya mapato na matumizi ya mwaka 2025/26, Prof.Mkenda amesema kwa mwaka wa kwanza watakaonufaika ni 88,320 na wanaoendelea 164,453 mwaka 2025/26.
Pia, amesema itaendelea kutoa mikopo kwa wanafunzi 10,000 wa ngazi ya stashahada katika fani za kipaumbele ikiwamo Sayansi, Teknolojia, Uhandisi na Hisabati.
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED