Katambi akabidhi kombati 100 kwa UVCCM

By Marco Maduhu , Nipashe
Published at 04:31 PM Mar 25 2025
Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Samweli Jackson (kulia), akikabidhi kombati 100 kwa Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, Abdulaziz Sakala, kwa ajili ya vijana wa Itifaki
Picha: Marco Maduhu
Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Samweli Jackson (kulia), akikabidhi kombati 100 kwa Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, Abdulaziz Sakala, kwa ajili ya vijana wa Itifaki

MBUNGE wa Jimbo la Shinyanga Mjini, Patrobas Katambi, ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana, Ajira na atu wenye ulemavu, amekabidhi kombati 100, kwa Itifaki ya Jumuiya ya Umoja wa Vijana UVCCM wilaya ya Shinyanga Mjini.

Kombati hizo zimekabidhiwa leo, Machi 25, 2025 na Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini, Samweli Jackson, kwa niaba ya Mbunge Katambi.

Samweli amesema vijana hao walimwomba Mbunge Katambi awapatie kombati hizo, kwa ajili ya shughuli za kichama na kwamba leo amezikabidhi rasmi, zenye thamani ya Sh. milioni 3.5.

Katambi akabidhi kombati 100 kwa UVCCM
“Mbunge Katambi ameahidi kuendelea kushirikiana na umoja huu wa vijana UVCCM na leo, amekabidhi maombi ya kombti 100 kwa Itifaki,” amesema Samweli.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana UVCCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, Abdulaziz Sakala, amemshukuru Mbunge Katambi kwa kutekeleza ombi lao, huku wakiahidi kuendelea kushirikiana naye katika shughuli za kichama, na hata kukipatia ushindi chama kwenye uchaguzi mkuu 2025, kwa kuchagua madiwani, wabunge na rais.CCM