Mamlaka nchini India yasitisha safari za ndege

By Enock Charles , Nipashe
Published at 11:26 AM May 10 2025
Ndege ya India
PICHA: MTANDAO
Ndege ya India

Mamlaka ya anga ya nchini India imesitisha safari za ndege kwa muda kutokana na mashambulizi ya makombora kutoka kwa jirani yake Pakistan huku pande zote zikishutumiana.

Televisheni ya taifa ya Pakistani na idara ya uhusiano wa umma ya jeshi zimesema kuwa mashambulizi dhidi ya India yameanzishwa, baada ya kuishutumu Delhi kwa kurusha makombora katika vituo vitatu vya ndege vya Pakistan.

Kwa mujibu wa Idara ya Mahusiano ya Umma ya Jeshi la Pakistani (ISPR), Pakistan imeita mashambulizi hayo ya kulipiza kisasi "Operesheni Banyan Marsus".

India haijatoa maoni yoyote kuhusu hatua hiyo.Maeneo yaliyoathirika na usitishaji huo nchini humo ni pamoja na Bathinda, Kandla, Sarasa, Uttarlai, Shimla, Ambala, Adhampur na Jamnagar