MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amegawa sadaka ya futari kwa wanawake zaidi ya 600 wenye mahitaji maalum kutoka Jumuiya ya Wanawake wa Kiislamu Tanzania (JUWAKITA), kuwawezesha kujikimu chakula katika kipindi cha mfungo wa mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
Mbali na hilo, ameagiza jumuiya hiyo kutumia hekma, busara na akili kubwa, ili kuweza kufikia malengo sahihi bila kuleta athari katika jamii hasa katika swala zima la kuongeza familia.
Ameyasema hayo leo, Machi 23, 2025 jijini Dar es Salaam, Makao Makuu ya Baraza la Waislamu Tanzania (BAKWATA) katika ugawaji sadaka ya futari kwa wanawake wenye uhitaji.
"Nyinyi wanawake mkisimama imara kama inavyotakiwa katika suala zima kufanya chaguzi na mtu ambae unaenda kuanzisha mahusiano basi naamini hili swala la watoto wa mitaani tutakwenda kulimaliza kwa asilimia mia," amesema.
Aidha amesema ugawaji futari umekuja baada ya kuona umuhimu mkubwa kuwagawia futari wanawake ambayo haijapikwa wakafuturu na walio nyuma yao wanaowategemea kuliko kuwaita mahali wafuturu wao pekee na nyumbani wameacha watoto na wanaowategemea.
Mufti amesema kuwa katika kipindi hicho kijacho cha uchaguzi kutazuka mambo mengi wasiyoitakia mema nchi na kuweza kupenya kwenye makundi na Jumuiya za wanawake, ili mradi kukosesha amani ya nchi.
"Nawausia akinamama achaneni na uzishi uzushi kwakuwa kipindi hiki wanafiki watu waongo waongo machawa watazuka sana kuwatumia ninyi wanawake kuishi kwa tahadhari kubwa kuendelea kuilinda amani yetu ya nchi," amesema Mufti.
Amesisitiza wanawake ni jeshi kubwa nchini, hivyo wasimame na kwenda kuchagua viongozi makini wa kuisogeza nchi mbele.
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED