WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu, Ridhiwani Kikwete, amepongeza Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), kuwajali watu wenye mahitaji maalum kwa kuwapa kipaumbele kama walivyo watumishi wengine.
Hayo ameyasema leo Aprili 29, 2025, mkoani Singida alipotembelea banda la WCF katika Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi, yanayoendelea mkoani humo.
Kikwete amekutana na kuongea na wafanyakazi wenye mahitaji maalumu ambao ni waajiriwa wa WCF na ameridhishwa na utendaji wao ambao umefanywa na mfuko huo.
“Nilipoanza kazi WCF, waliniuliza vifaa ninavyohitaji katika kutekeleza majukumu yangu, niliwaeleza na nilipatiwa vifaa hivyo na kwa sasa ninaendelea kutekeleza majukumu yangu kikamilifu”
Pia, Kikwete amesema jitihada za kuimarisha usawa na ujumuishaji mahali pa kazi zinaonekana na kusisitiza umuhimu wa kuendelea kutoa elimu na huduma bora zaidi kwa wafanyakazi wote.
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED