Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira amewataka wananchi mkoani Kagera kutumia rasilimali zilizopo mkoani humo ikiwemo mifugo ya ng'ombe ili kujiinua kiuchumi.
Amebainisha hayo wakati akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Viwanja vya Kemondo Center ndani ya Tarafa ya Katerero Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba.
"Kama familia zinaweza kufanya ufugaji wa ng,ombe kila kaya hata ng'ombe wawili hizo familia zikawa na uhakika wa kupata maziwa na kikawepo kiwanda cha maziwa familia zinaweza kupata pesa na kujiokoa na umasikini," amesema Wasira.
Kadhalika, Wasira amesema serikali imetoa Sh.bilioni 106.4 kufanikisha miradi ya maji, afya, barabara, umeme na elimu katika Jimbo la Bukoba Vijijini mkoani Kagera kwa kipindi cha miaka minne.
Amesema kupitia Vyuo vya Ufundi Stadi (VETA) itaendelea kujenga vyuo hivyo kila wilaya ili kuendelea kutoa uzoefu kwa vijana wengi Mkoa wa Kagera kuendelea kujiajili na kuajiliwa huku akiwataka viongozi waliopewa dhamana na wananchi wao kuendelea kufanya ubunifu wa kuwangunisha katika mifumo ya kuwapatia vijana pesa ya haraka kama mifugo na uvuvi.
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED