Waziri Ridhiwani Kikwete afurahishwa na jinsi PSSSF inavyohudumia wanachama

By Mwandishi Wetu , Nipashe
Published at 09:01 PM Jul 04 2025
Waziri Ridhiwani Kikwete afurahishwa na jinsi PSSSF inavyohudumia wanachama
Picha:Mpigapicha Wetu
Waziri Ridhiwani Kikwete afurahishwa na jinsi PSSSF inavyohudumia wanachama

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Ridhiwani Kikwete ametembeela banda la Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma PSSSF kwenye Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam na kujionea jinsi wanachama na wananchi wanavyohudumiwa.

Kikwete ambaye aliambatana na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu,Patrobas Katambi, Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Zuhra Yunus, alielezwa jinsi wanachama na wananchi wanavyohudumiwa katika banda hilo.

Amefurahishwa na taarifa ya namna wanachama wanavyofurahia huduma za PSSSF Kidijitali ambazo zimepelekea mapinduzi makubwa katika utoaji wa huduma. 

Pia Mhe. Kikwete alijionea bidhaa bora za viatu, mikoba na mikanda vinavyozalishwa kwenye kiwandha cha KLICL  ambacho PSSSF imewekaza.

Halikadhalika alijionea nyama safi inayotoka kwenye Machinjio ya Kimataifa ya Nguru Hills Ranch, ambayo PSSSFni muwekezaji mkubwa.