Ukraine ilivyofanikisha shambulizi Kilometa 4300 ndani ya Urusi

By Enock Charles , Nipashe
Published at 09:19 AM Jun 02 2025
Ukraine ilivyofanikisha shambulizi Kilometa 4300 ndani ya Urusi
Picha:Mtandao
Ukraine ilivyofanikisha shambulizi Kilometa 4300 ndani ya Urusi

Jana Ukraine iliweka historia mpya katika uwezo wake wa kijeshi baada ya kufanikiwa kufanya shambulizi kubwa ndani kabisa ya Urusi.

Ukraine ilishambulia ndege za kivita za Urusi zilizo umbali wa kilometa 4300 yaani ni sawa na umbali wa kutoka Dar es Salaam hadi Afrika Kusini.

Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa wa Ukraine, Vasyl Malyuk ameeleza jinsi ilivyokuwa vigumu kufanya shambulizi hilo lililofanyiwa utafiti kwa zaidi ya Mwaka mmoja na nusu kabla ya kutekelezwa huku likisimamiwa na Rais Volodomyr Zelensky yeye mwenyewe.

Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa wa Ukraine, Vasyl Malyuk.

Shambulizi hilo lilifanikiwa kuharibu ndege 40 za kivita za Urusi zilizokuwa katika Uwanja wa ndege wa kijeshi ndani kabisa ya Urusi ili kuzificha dhidi ya mashambulizi ya Ukraine ambayo mara nyingi yaligusa mikoa ya mpakani mwa Urusi na Ukraine.