Kamati yakagua ujenzi wa nyumba 101

By Beatrice Moses , Nipashe
Published at 06:11 PM Apr 17 2025
Kamati yakagua ujenzi wa nyumba 101
Picha: Beatrice Moses
Kamati yakagua ujenzi wa nyumba 101

KAMATi ya Bodi ya ya Uwekezaji na Fedha ya Watumishi Housing Investment, imekagua mradi wa Nyumba 101 zinazojengwa Dar es Salaam, kwa ajili ya kuwauzia watumishi wa umma.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Celestine Muganga, amesema wameridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mradi huo, unavyoendelea, hatua ambayo inaonyesha juhudi za kufanikisha lengo lilowekwa na kuwawezesha watumishi wa umma kumiliki nyumba  bora zinazojengwa chini ya WHI. 

Meneja Maimamizi.wa mradi huo Msanigu ujenzi Yusuph Mlimakifi amesema hadi Sasa mradi huo umefika asilimia.20  ulianza Seotemba 2024 unapaswa kukamilika Machi 2026. 

Kamati yakagua ujenzi wa nyumba 101
Nyumba hizo zenye thamani ya shilling bilioni 18.6 zinajengwa Mikocheni Regent Estate, Dar es Salaam. 

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa WHI, Sefania Solomon, amesema wamekusudia kuendelea kutekeleza miradi mingine kadhaa katika maeneo tofauti nchini, ili kufanikisha watumishi wa umma wenye nia ya kumiliki nyumba. 

Mwakilishi ya  kampuni ya  ujenzi ya kimataifa ya Shadong Hi- Speed Group Wang Younsheng  amesema wamekusudia kuhakikisha 

Jengo hilo lenye ghorofa 12 linajengwa kwa viwango vinavyotakiwa na linakamilika kwa wakati.