KATIBU wa CHADEMA Jimbo la Iringa, Paschal Chibala, ametangaza sababu zilizomfanya kuhama chama chake na kukimbilia Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Chibala ametangaza leo kuhamia CCM wakati wa mkutano wa hadhara wa Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa, CPA Amos Makalla, ambaye amehitimisha ziara yake ya siku tatu katika mikoa ya Mbeya na Iringa.
Akizungumza baada ya kupokewa na CPA Makalla katika mkutano huo uliofanyika uwanja wa Mwembetogwa, mkoani Iringa, Chibala ametaja sababu ni baada ya kuona alikokuwa hawana sera.
Amedai kuwa CHADEMA wanatembea kwa kuwadanganya wananchi no reform.
Kadhalika ametaja sababu nyingine ni wakati Mchungaji Peter Msigwa, akiwa CHADEMA alimpelekea Mwenyekiti ambaye anadai hajui kusoma wakati yeye ana Degree (Shahada).
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED