Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Anamringi Macha, akizungumza na watoto wanaolelewa katika Kituo cha Kulelea Watoto Yatima cha Mvuma, kilichopo Kata ya Nyasubi, manispaa ya Kahama, leo
RAIS Samia Suluhu Hassan, ametoa sadaka ya mahitaji mbalimbali, kwa watoto yatima na wanaotoka katika mazingira magumu wapatao 227, wilayani Kahama, mkoani Shinyanga, kwa vitu vyenye thamani ya zaidi ya Sh. milioni tano.
Lengo ni kusherehekea kwa pamoja sikukuu ya Eid-Al-Fitri.Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Anamringi Macha, akikabidhi mbuziWatoto hao wanatoka katika vituo vya kulelea yatima vya Mvuma kata ya Nyasubi, Zaqalinah Kata ya Kagongwa; New Hope mtaa wa Mwime Kata ya Zongomela pamoja na Kituo cha Kahama Peace kilichopo mtaa wa Dodoma Kata ya Zongema, manispaa ya Kahama.
Amesema kila mwaka Rais Samia Suluhu Hassan, amekuwa akila sikukuu pamoja na watoto yatima, wajane na wanaotoka katika mazingira magumu, kwa kuwapatia mahitaji mbalimbali na muhimu na kuwataka wengine kufanya hivyo.Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Anamringi Macha (kulia) akishirikiana na Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Mboni Mhita (kushoto), kukata kutoweoOfisa Ustawi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kahama, Swaiba Chemchem, amesema watoto 227 wamefikiwa na sadaka kati yao 35 wanatoka kituo cha Mvuma, 32 Zaqalinag, 75 New Hope pamoja na 85 Kahama Peace.
Pia amesema, kituo cha New Hope kimekuwa kikipokea watoto wengi kutoka Msalala, Ushetu na manispaa hiyo, wakiwamo wanaotoka nchi jirani ya Burundi, ambao baadae wanarejeshwa nchini mwao.Picha ya pamoja ya watoto yatima na viongozi mbalimbali wa wilaya na mkoa wa ShinyangaAkizungumza kwa niaba ya wamiliki wa vituo hivyo, Mkurungezi wa New Hope, Suleimani Nkanda, amemshukuru Rais Samia, kwa mahitaji hayo na kuahidi kutumika kwenye matumizi yaliyopangwa.