VIONGOZI wa umma wametakiwa kuongoza nchi kwa haki na kuimarisha upendo kwa jamii, ili kumuenzi aliyekuwa Rais wa Tanzania, Hayati Dk. John Pombe Magufuli (JPM).
Magufuli, alifariki dunia Machi 17, 2021 wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Mzena, Dar es Salaam.
Amesema, wale waliochukizwa na kwa namna yoyote na utawala wake wamsamehe kwa kuwa ndiyo siri ya kuvuna baraka za Mwenyezi Mungu.
"Dk. Magufuli alikuwa ni mwanadamu na kwa niaba yake mimi ninaomba kwa mabaya yoyote aliyotenda tumsamehe maana hayupo tena duniani na wasioweza kumsamehe mimi ninasema, hao siyo wakristo" amesema Askofu Niwemugizi.
Pamoja na mambo mengine, amesisitiza kila mmoja kuandika kitabu chake vizuri kingali bado hai, huku akisisitiza kuwa kila mwaka kanisa litaendelea kumwombea Hayati Magufuli, kutokana na mchango wake mkubwa kwa kanisa na taifa kwa ujumla.
Kadhalika amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan, kwa kutuma uwakilishi wake katika ushiriki wa maadhimisho ya ibada hiyo na kwamba Watanzania wanapaswa kuendelea kuishi kwa upendo na mshikamano.
"Tunayakumbuka maisha ya Hayati Dk. Magufuli, kwa mambo mengi aliyotenda enzi za uhai wake, maana alitambua na wakati wote alisisitiza maneno tumtangulize Mungu na tumrudie Mungu.
“Ndiyo maana tunamwombea yeye pamoja na viongozi walioko madarakani, kwa maana watu wanataka waishi kwa amani na utulivu," amesema Askofu Niwemugizi.
Katika ibada hiyo, viongozi mbalimbali wa chama na serikali wamehudhuria, akiwamo mwakilishi wa Rais Samia, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu, William Lukuvi, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa.
Wengine ni Mkuu wa Mkoa wa Geita, Martine Shigela, Makamu Mwenyekiti UVCCM Taifa, Rehema Sombi na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita, Elias Kasendamila na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Geita, Robert Gabriel Luhumbi.
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED