Jumla ya makosa 1,197 ya jinai yameripotiwa Zanzibar katika kipindi cha Januari hadi Juni, 2025, yakionesha upungufu wa makosa 455 ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka jana ambapo yalikuwa 1,652, sawa na asilimia 27.7.
Kamishna wa Polisi Zanzibar, Kombo Khamis Kombo, amesema hayo leo Agosti 1, 2025, wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Zanzibar.
"Kupungua kwa makosa haya kunatokana na juhudi za pamoja za kutoa elimu kwa jamii kupitia ngazi za shehia, vyombo vya habari na kampeni mbalimbali za uhamasishaji ambazo zimeongeza uelewa wa wananchi kuhusu madhara ya uhalifu," amesema Kamishna Kombo.
Amesema kati ya makosa 1,197 yaliyoripotiwa, makosa dhidi ya binadamu yalikuwa 409, yakionesha upungufu wa makosa 202 kutoka makosa 611 yaliyotokea mwaka jana – sawa na asilimia 33.1.
Makosa hayo ni pamoja na:
Kamishna Kombo amesema aina nyingine za makosa yaliyosajiliwa ni pamoja na:
Akifafanua kuhusu kesi za mauaji 26, Kamishna Kombo alisema asilimia 3 ya matukio hayo yamesababishwa na wivu wa kimapenzi, huku asilimia 6 yakitokana na ugomvi katika vilabu vya starehe. Sababu nyingine zinaendelea kuchunguzwa.
"Jeshi la Polisi litaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kutoa elimu ya kupinga vitendo vya jinai na kuhakikisha Zanzibar inabaki kuwa mahali salama kwa wananchi na wageni," ameongeza Kombo.
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED