TANZANIA leo, imetangaza kumalizika kwa mlipuko wa ugonjwa wa virusi vya Marburg, baada ya kutoripotiwa kwa kesi mpya kwa zaidi ya siku 42 tangu kifo cha mgonjwa wa mwisho, aliyethibitishwa Januari 28, mwaka huu.
Hayo ni kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), na kwamba mlipuko huo ambao ulisababisha kesi mbili zilizothibitishwa na zingine nane zinazoshukiwa (wote walifariki), ulikuwa wa pili kutokea nchini.
Mlipuko huo, uliitangazwa Januari 20, 2025 na ule wa mwaka 2023, yote ilitokea katika mkoa wa Kagera, kaskazini mashariki mwa Tanzania.
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED