MKURUGENZI wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela Ummy Wayayu ametoa madawati 25 kwa shule ya msingi Mnarani iliyoripotiwa kuwa na upungufu wa madawati ili kuhakikisha wanafunzi hao wanasoma katika mazingira ya kisasa na yaliyobora.
Akimkabidhi madawati hayo kwa Mkuu wa shule hiyo Wayayu leo amesema lengo la serikali ni kuona wanafunzi wanasoma katika mazingira yaliyo bora na yenye kuleta tija.
Mkuu wa shule hiyo Dismas Hamaro amemshukuru Mkurugenzi huyo kwa kuipatia shule madawati hayo ambayo yatasaidia wanafunzi kukaa vizuri na kuweza kujifunza vizuri.
Aidha ameahidi ya kutunza miundo mbinu hiyo ya madawati vizuri ili inufaishe vizazi vingi vitakavyopita shuleni hapo na viweze kujifunza kwa ufanisi.
"Shule yetu ina wanafunzi 818 ambako kumekuwa na ongezeko kubwa la wanafunzi walioandikishwa darasa la awali na darasa la kwanza 2025 kutokana na sera ya Elimu bila malipo na hivyo jamii imekuwa na mwamko mkubwa wa kuandikisha watoto,” amesema Hamaro.
Aidha ametaja kuwa ongezeko hilo limesababisha shule kuwa na upungufu wa madawati na kuwa wamepokea madawati kutoka kwa Mkurugenzi na wadau mbalimbali akiwemo Desk and Chair Foundation Tanzania hivyo kubaki na upungufu wa madawati 26 pekee.
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED