Mgombea Urais wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Salum Mwalimu, amesema serikali yake itaanzisha mfuko maalumu kwa ajili ya kusaidia, kusimamia na kuendeleza mawazo ya kibiashara ya vijana nchini.
Akizungumza leo mjini Geita katika mkutano wa kampeni, Mwalimu alisema lengo ni kuhakikisha hakuna biashara ya kijana inayokufa chini ya uongozi wake.
Ameongeza kuwa serikali yake itashirikiana na wawekezaji kutengeneza mfuko maalumu wa kuratibu na kusimamia matumizi ya mapato ya Mfuko wa Jamii wa Makampuni Makubwa (CSR), ili fedha hizo zisitumike vibaya.
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED