Tanzania, Italia zasaini makubaliano ushirikiano kwenye ulinzi

By Mwandishi Wetu , Nipashe
Published at 05:25 PM Mar 29 2025
Tanzania, Italia zasaini makubaliano ushirikiano kwenye ulinzi
Picha: Mpigapicha Wetu
Tanzania, Italia zasaini makubaliano ushirikiano kwenye ulinzi

PEMBEZONI mwa Mkutano wa Mpango wa Mattei kwa Afrika na ‘EU Global Gateway’ jijini Roma, Italia, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi, Mahmoud Thabit Kombo;

Amekutana na Waziri wa Ulinzi wa Tanzania, Stergomena Tax aliyekuwa kwenye ziara ya kikazi nchini humo, Tanzania na Italia zimesaini Hati ya Ushirikiano katika Masuala ya Ulinzi.

Kwa pamoja viongozi hao walifanya kikao cha pamoja na watumishi wa wizara walioambatana nao, watumishi na watendaji wa Ubalozi wa Tanzania nchini Italia pamoja na wawakilishi wa Diaspora ya Watanzania waishio Italia.