MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Stephan Wasira, amewataka wanachama wa chama hicho kuwa wasiogope kwakuwa hakuna chama kinachowasumbua na wanaosubiri kwamba kitaanguka watasubiri sana.
Akizungumza na wanachama wa CCM Mkoa wa Tabora leo, ambako yuko katika ziara ya kikazi Wasira amesema wanaosubiri CCM itakufa watasubiri sana kwasababu kina mizizi iliyojichimbia chini na inasambaa katika kila nyumba, hivyo viongozi wajisifie chama chao.
"Chama cha namna hiyo huwezi kukiua kwa sababu wenyewe wako kila nyumba 10, wanaobeza chama muwasamehe maana hawajui wanachokifanya, CCM nichama kikubwa Tanazania na Afrika kwa ujumla," amesema Wasira.
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED