Derby ya Kariakoo kati ya Yanga na Simba ni moja ya mechi kubwa zaidi nchini, ikijaa ushindani ndani ya uwanja na tambo kutoka kwa mashabiki wa timu hizo mbili za mtaa wa Kariakoo.
Hapa ni nyota wa kutazama kwenye derby hii.
Tangu ajiunge na Simba, Kibu amekuwa mwiba hasa kwenye mechi za watani wa jadi. Katika derby alizocheza, amefanikiwa kufunga mabao mawili. Katika mchezo wa mwisho, alichezewa faulo nyingi kuliko mchezaji yeyote uwanjani.
Mmoja wa wachezaji hatari anapopata nafasi ya kushambulia. Mikimbio yake na uwezo wa kupunguza wachezaji zaidi ya mmoja huleta tishio langoni kwa wapinzani.
Hii itakuwa derby yake ya kwanza tangu ajiunge na Simba dirisha dogo. Ameonyesha uwezo mkubwa na anatarajiwa kuwa mwiba kwa wapinzani kutokana na uwezo wake wa kupandisha mashambulizi.
Tayari ameshafunga bao katika mechi za watani wa jadi. Uchezaji wake umekuwa bora sana, na anatarajiwa kuwa miongoni mwa wachezaji hatari katika mchezo huu.
Hajacheza derby nyingi, lakini ni mchezaji mwenye rekodi nzuri ya kufunga dhidi ya Simba, akiwa amewafunga alipokuwa Azam FC. Anaweza kuleta tofauti katika mchezo huu.
Si mchezaji anayeimbwa sana, lakini ana uwezo mkubwa. Kasi yake na pressing zinaweza kuleta kitu tofauti. Katika derby yake ya kwanza hakufunga, lakini alionekana kuwa tishio kubwa.
Kipaji kikubwa na mchezaji muhimu wa kuichezesha timu. Uwezo wake wa kupiga mashuti na kutoa pasi za mwisho unamfanya kuwa hatari anapokaribia eneo la 18 la mpinzani.
Si mchezaji anayezungumziwa sana, lakini ni hatari katika mipira iliyokufa. Anaweza kuadhibu wapinzani au kusababisha timu yake kuadhibiwa.
Katika derby yake ya kwanza, alikosa nafasi ya wazi ambayo ingeweza kumweka kwenye rekodi ya wafungaji wa mechi za watani wa jadi. Uwezo wake wa kusimama na mabeki zaidi ya wawili unaweza kufungua mianya kwa wachezaji wenzake.
🔜 #DerbyYaKariakoo | #YangaVsSimba | #NBCPL
✍🏽 Mwakalobo Jnr.
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED