EWURA yatoa vibali 182 mijini, 26 vijijini miundombinu ya mafuta

By Mwandishi Wetu , Nipashe
Published at 07:20 PM Apr 30 2025
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk Doto Biteko.
Picha: Mtandao
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk Doto Biteko.

Kufikia Aprili 2025, EWURA ilitoa jumla ya vibali 215 vya ujenzi wa miundombinu ya mafuta ambapo vibali 182 vilitolewa kwa vituo vya mjini na vibali 26 kwa vituo vya vijijini.

Aidha, vibali vitano (5) vilitolewa kwa ajili ya miundombinu ya kuhifadhi mafuta kwa watumiaji wakubwa kama vile viwanda na migodi, na vibali viwili (2) kwa ajili ya maghala ya kuhifadhi na kujaza LPG.

Kazi nyingine zilizotekelezwa na EWURA ni kusimamia taratibu za uagizaji na usambazaji wa mafuta nchini; na kusimamia ubora wa bidhaa za mafuta ambapo jumla ya sampuli 334 kutoka katika vituo vya mafuta na maghala zilipimwa ubora na sampuli 321 sawa na asilimia 96.1 zilikidhi viwango stahiki vya ubora.

Taratibu za kisheria zilichukuliwa kwa vituo ambavyo vilibainika kuwa na mafuta yasiyokidhi viwango vya ubora. Aidha, EWURA ilikagua ubora wa miundombinu  569  ya  mafuta​ambapo miundombinu 451 sawa na asilimia 76.2 ilikidhi viwango vya ubora ikiwemo vigezo vya masuala ya afya, usalama na mazingira.

#Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Nishati 2025/26