Ajali ya ‘ambulance’ na toyo yaua saba

By Mwandishi Wetu , Nipashe
Published at 05:22 PM Apr 19 2025
Ajali ya ambulance na toyo huko Mafinga
PICHA: MARY SANYIWA
Ajali ya ambulance na toyo huko Mafinga

Watu saba wamefariki dunia, huku wengine 15 wakijeruhiwa baada ya ajali kutokea ikihusisha gari la kubeba wagonjwa (ambulance) na toyo huko Luganga, Mafinga mkoani Iringa.

Akizungumza kutokea eneo la ajali alipokuwa akitembelea majeruhi, Mkuu wa Wilaya ya Mufindi, Dk Linda Salekwa amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo akisema taarifa zinaonesha watu waliokuwa katika toyo hiyo walikuwa wanakwenda shambani.