Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya, limethibitisha kuwa mtoto Devina Derick (2), mkazi wa Kijiji cha Isaka, Rungwe, aliuawa kwa kunyongwa na baba yake mzazi, Derick Mwangama (23), kwa kutumia kamba ya manila.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, SACP Benjamin Kuzaga, amesema tukio hilo limetokea Novemba 18, 2025, baada ya mtuhumiwa kumchukua mtoto kwa nguvu kutoka kwa mama yake, Violeth Edward (19), kabla ya kutoweka naye na mwili wa Devina ulipatikana kando ya Mto Kiwira baada ya msako wa wananchi na polisi.
Kamanda Kuzaga ameeleza kuwa baada ya mtuhumiwa kutekeleza mauaji ya mwanae nae alikutwa amejinyonga kwenye mti wa mparachichi karibu na alipotupa mwili wa mtoto.
Kamanda Kuzaga amesema uchunguzi wa awali unaonyesha chanzo cha tukio ni mgogoro wa kifamilia, amewataka wazazi wenye matatizo kutafuta suluhu kwa njia za kisheria na majadiliano ya amani ili kuepusha madhara kama hayo.
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED