Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesitisha mara moja ziara, mikutano, semina na makongamano, yanayohusisha wajumbe wa vikao vinavyopigia kura za maoni wagombea kwa ngazi zote mpaka baada ya kura za maoni.
Kwa mujibu wa taarifa kwa umma iliyotolewa na Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi vikao hivyo ni kwa nafasi za ubunge, uwakilishi na udiwani ambavyo vimekuwa vikiendelea kwenye maeneo mbalimbali.
“CCM inaendelea kusisitiza kuwa mwanachama yeyote anayetarajia kugombea au wakala wake kuepuka kufanya vitendo vyovyote vinavyoonekana dhahiri kuwa ni kinyume cha katiba, kanuni na miongozo ya chama chetu,”amesema Balozi Nchimbi.
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED