CHAUMMA yakiri kuiona barua ya Kabendera

By Grace Mwakalinga , Nipashe
Published at 04:32 PM May 27 2025
Eugene Kabendera.
Picha: Mpigapicha Wetu
Eugene Kabendera.

Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), kimekiri kupokea taarifa ya kujiuzuru kwa aliyekuwa mwanachama wake, Eugene Kabendera, kupitia vyombo mbalimbali vya habari na mitandao ya kijamii.

Akizungumza kwa niaba ya chama, Naibu Mkurugenzi wa Idara ya Mawasiliano na Uenezi, Ipyana Samson, amesema chama kinatambua mchango mkubwa alioutoa Kabendera katika kipindi alichokuwa ndani ya chama hicho.

“Tumeona barua yake ambayo imesambaa mitandaoni, tunamtakia kila la heri huko aendako. CHAUMMA sasa kinaelekeza nguvu zake zote kwenye maandalizi ya tukio kubwa la uzinduzi wa Oparesheni CHAUMMA for Change (C4C), linalotarajiwa kufanyika Mwanza, Juni 1, 2025,” amesema Samson.

Kabendera alikuwa miongoni mwa wanachama waliowahi kushika nyadhifa mbalimbali ndani ya chama hicho na kuchangia katika kukijenga.