Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) limetangaza rasmi nafasi za vijana waliohitimu kidato cha sita mwaka 2025 kutoka shule mbalimbali nchini, kujiunga na mafunzo ya kijeshi kwa mujibu wa sheria, kuanzia kesho Mei 28 hadi Juni 8, 2025.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dodoma, Kaimu Mkuu wa Tawi la Utawala wa JKT, Kanali Juma Mlay, amebainisha kuwa vijana walioteuliwa wanapaswa kuangalia majina yao pamoja na kambi walizopangiwa kupitia tovuti rasmi ya Jeshi la Kujenga Taifa: www.jkt.mil.tz.
Kanali Mlay amesisitiza kuwa nafasi hizo hutolewa bure na ametoa tahadhari kwa jamii kuepuka kudanganywa na matapeli wanaojifanya wasaidizi wa upatikanaji wa nafasi hizo. “Tovuti rasmi ya JKT ndiyo chanzo pekee cha taarifa sahihi. Hakuna ada yoyote inayotozwa,” aliongeza.
Baadhi ya kambi ambazo vijana wanapaswa kuripoti ni:
Kwa vijana wenye ulemavu wa kuona, wanapaswa kuripoti katika kambi ya JKT Ruvu, mkoani Pwani, kwa ajili ya mafunzo yao maalum.
Kanali Mlay ameeleza kuwa vijana wote wanapaswa kuripoti wakiwa na vifaa vifuatavyo:
Kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa, Meja Jenerali Rajabu Mabele, Kanali Mlay ametoa wito kwa vijana wote waliomaliza kidato cha sita mwaka huu, kutoka shule za Tanzania Bara, kuhudhuria mafunzo hayo muhimu kwa mujibu wa sheria.
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED