Kinabo: CHAUMMA tutajenga viwanda zaidi ya 20 vya kubangua korosho

By Elizabeth Zaya , Nipashe
Published at 03:43 PM Jul 16 2025
Mkurugenzi wa Itikadi, Mafunzo na Oganizesheni wa CHAUMMA, Edward Kinabo.
Picha: Mpigap
Mkurugenzi wa Itikadi, Mafunzo na Oganizesheni wa CHAUMMA, Edward Kinabo.

"CHAUMMA tutajenga viwanda vya kubangua korosho zaidi ya 20. Sera yetu haiishii tu kwenye kuchochea viwanda, itahakikisha mkulima mmoja anapata mashine ndogondogo zenye teknolojia rahisi ili kila mkulima abangue mweyewe na kuziua zikiwa zimebanguliwa na kunufaisha.

"Kwa hiyo CHAUMMA itapiga hatua moja mbele kunyanyua kilimo na kuipandisha thamani ya korosho, tukifanya hivi tutainua kipato na kuboresha maisha ya wananchi." Amesema Mkurugenzi wa itikadi, Mafunzo na Oganizesheni.

Amesema asilimia 90 ya korosho inayouzwa haijabanguliwa.

"Na ikiuzwa hivyo bila kiwango, haina faida kwa wakulima, kwa hiyo kama kungekuwa na viwanda vya kutosha vya kubangua Korosho, wakulima wote wangeuza korosho ikiwa imebanguliwa"

"Kilo moja ya Korosho iliyobanguliwa ni zaidi ya sh.10,000 na isiyobanguliwa ni sh.4000 katika kila kilo akiuza isiyobanguliwa anapoteza zaidi ya sh.6000."