Ushahidi wa siri wakwamisha kesi ya Boni Yai, Malisa

By Imani Nathaniel , Nipashe
Published at 12:10 PM Jul 16 2025
Ushahidi wa siri wakwamisha  kesi ya Boni Yai, Malisa
Picha:Imani Nathaniel
Ushahidi wa siri wakwamisha kesi ya Boni Yai, Malisa

Kesi ya kuchapisha taarifa za uongo kwenye mitandao ya kijamii inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Pwani, Boniphace Jacob, pamoja na Afisa wa masuala ya Haki za Binadamu, Godlisten Malisa imetajwa leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam.

Washatakiwa hao wanatetea kupitia wakili wao, Dickson Matata, huku kesi hiyo ikiwa katika hatua ya usikilizwaji wa mashahidi.

Awali, mawakili wa Jamhuri waliwasilisha ombi la mashahidi kusikilizwa kwa siri, lakini mahakama ililikataa. Hata hivyo, upande wa Jamhuri ulikata rufaa Mahakama Kuu, na uamuzi wa rufaa hiyo bado unasubiriwa.

Kesi imepangwa kutajwa tena tarehe 4 Septemba mwaka huu saa 5:00 asubuhi.