Kishindo cha Sabaya siasa za Arusha

By Godfrey Mushi , Nipashe
Published at 11:59 AM Jul 01 2025
Lengai Ole Sabaya akichukua fomu.
Picha: Mpigapicha Wetu
Lengai Ole Sabaya akichukua fomu.

Ni yule yule, Lengai Ole Sabaya, unayemjua katika ulingo wa siasa za kaskazini mwa Tanzania, amerejea tena.

Sasa ni rasmi, analitaka Jimbo la Arumeru Magharibi, mkoani Arusha.

Baada ya Ole Sabaya, kuchukua fomu ya kuomba kugombea nafasi ya uongozi katika vyombo vya dola, leo asubuhi saa 4:38 ya Julai 1, 2025, amesema neno moja 'Namuachia Mungu afanye kazi yake"

Ole Sabaya, aliteuliwa kwa mara ya kwanza kuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, mkoani Kilimanjaro, Julai 28,2018.

Pia, amewahi kuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM), Mkoa wa Arusha na Diwani wa Kata ya Sambasha, Halmashauri ya Arusha.

1