Rais aridhia msamaha faini zote za maji kwa wananchi wenye madeni

By Paul Mabeja , Nipashe
Published at 01:21 PM May 08 2025
Waziri wa Maji Juma Aweso.
Picha: Ibrahim Joseph
Waziri wa Maji Juma Aweso.

Waziri wa Maji Jumaa Aweso, amesema Rais Samia Suluhu Hassan, ameridhia msamaha wa faini zote kwa wananchi wenye madeni ya maji katika mamlaka mbalimbali nchini.


Aweso amesema hayo leo Bungeni jijini Dodoma wakati akiwasilisha makadilio ya Bajeti ya Wizara yake katika mwaka wa fedha 2025/2026. 

“Katika hatua ya kugusa moja kwa moja maisha ya wananchi, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, ameridhia msamaha wa faini zote kwa wananchi wenye madeni ya maji katika Mamlaka mbalimbali. 


“Mama Samia amesamehe fine hizo, hivyo wafike kwenye Mamlaka kwa ajili ya utaratibu wa kurejeshwa huduma ya maji hadi tarehe 31 Mei 2025.”amesema Aweso
 

Aidha, kwa wateja wote wenye madeni, Waziri Aweso amesisitiza kuwa ni fursa ya kipekee kwao kufika ofisi za Mamlaka za Maji kupewa utaratibu wa kulipa madeni hayo na kurejeshewa huduma mara moja bila usumbufu.