Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Samia Suluhu Hassan, amesema sekta ya madini imeendelea kuwa kinara katika kuchangia makusanyo ya Serikali, pato la wananchi na uwekezaji kwenye huduma za kijamii kama elimu na afya, hatua iliyochochewa na ongezeko la mchango wake kwenye Pato la Taifa kutoka asilimia 6.8 mwaka 2020 hadi 10.1 mwaka 2024.
Akizungumza leo Novemba 14, 2025, wakati akihutubia kwenye ufunguzi wa Bunge la 13 jijini Dodoma, Rais Samia ameeleza kwamba mageuzi na mikakati mipya imeiweka Tanzania kwenye mwelekeo thabiti wa kuwa kitovu cha biashara ya madini Afrika Mashariki na Kati ifikapo mwaka 2030.
Rais amesema mfuko huo utawekwa mahsusi kuhifadhi fedha zitokanazo na madini ili kuwapatia manufaa vizazi vijavyo, badala ya kuviachia vizazi hivyo mashimo yasiyo na tija.
Serikali itaruhusu mali za madini kutumika kama dhamana ya mikopo ya uwekezaji ili kuongeza mtaji kwa wachimbaji na kuongeza ufanisi katika sekta hiyo.
Ifikapo mwaka 2030 Tanzania inatarajiwa kuwa eneo kuu la biashara ya madini kutokana na wingi na utofauti wa rasilimali hizo nchini.
Kiwanda hicho kitaanza kufanya kazi mwaka 2030 ili kuongeza thamani ya madini hapa nchini, kuzuia usafirishaji wa makinikia nje na kuongeza ajira.
Serikali itaongeza kiwango cha utafiti kutoka asilimia 16 ya sasa ili kubaini hifadhi halisi ya madini na kuratibu kwa umakini uwekezaji katika maeneo yenye mahitaji makubwa ya kimataifa.
Kongani hiyo itajikita katika uzalishaji wa vipuri na bidhaa mbalimbali za madini, hatua inayolenga kujenga nchi inayojiamini kiutengenezaji.
Mkakati huo utaainisha aina za madini, maeneo yalipo, kiasi chake na namna ya kuyasimamia ili kuongeza tija ya kiuchumi.
BoT itaendelea kununua dhahabu kutoka kwa wachimbaji wadogo na wa kati wenye leseni ili kuimarisha akiba ya taifa, kurasimisha biashara na kupunguza utoroshaji.
Serikali imeahidi kukamilisha jengo hilo ili kuwezesha biashara ya tanzanite kufanyika kwa uwazi, ufanisi na kwa masoko ya kimataifa.
Masoko hayo yataimarishwa ili kuongeza thamani na kupanua wigo wa biashara ndani na nje ya nchi.
Serikali itapitia upya leseni zote zinazodumaa na kuzipatia wanaoweza kuzifanyia kazi ili kuongeza uzalishaji.
Rais Samia amesema Serikali itaendelea kuwapatia wachimbaji wadogo maeneo mapya, mitambo na taarifa sahihi za kijiolojia ili kuwawezesha kuendesha shughuli zao kisasa.
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED