Wananchi wahamasishwa umuhimu wa chanjo

By Gideon Mwakanosya , Nipashe
Published at 02:14 PM Jun 28 2025
Chanjo
PICHA: MTANDAO
Chanjo

Wananchi wilayani Songea Mkoa wa Ruvuma wamehamasishwa kutambua huduma muhimu za chanjo katika kuokoa maisha ya mtu mmoja mmoja na Jamii kwa ujumla ili kuwapatia taarifa sahihi za utoaji wa huduma za chanjo hapa Nchini na kuwaomba viongozi waendelee kusaidia kuhamasisha na kuelimisha Jamii kuhusu huduma hiyo katika kupinga magonjwa na kuzuia vifo.

Hayo yamesemwa na Kaimu Mkurugenzi wa idara ya kinga  Wizara ya Afya Dr Otilia Gowele kwenye mafunzo ya uhamasiaha  wa chanjo Mkoani Ruvuma  yaliyofanyika mwishoni mwa wiki kwenye ukumbi wa mikutano uliopo shule ya Sekondari Maposeni halmashauri ya songea ambao umehudhuriwa pia na viongozi mbalimbali wa halmashauri hiyo.
Naye Kaimu meneja mpango wa Taifa wa chanjo kutoka wizara ya  Afya Dr Georgina Joachim kwenye mkutano huo alitoa wito kwa wazazi na walezi  kuwapeleka watoto wao  wa kike wenye umri wa kuanzia miaka tisa hadi miaka kumi na minne kupatiwa chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi kwa kuwa tatizo hilo kwa sasa ni kubwa nchini huku akiwaomba kupinga mila potofu  zinazoenezwa na baadhi ya watu kuwa chanjo hizo zina madhara kiafya jambo ambalo sio la kweli.