Warioba: Sarungi alisaidia kumaliza mgomo wa wanafunzi UDSM

By Halfani Chusi , Nipashe
Published at 01:32 PM Mar 10 2025
Waziri Mkuu Mstaafu, Joseph Warioba.
Picha: Mpigapicha Wetu
Waziri Mkuu Mstaafu, Joseph Warioba.

Waziri Mkuu Mstaafu, Joseph Warioba, amesema Prof. Philemon Sarungi alikuwa miongoni mwa viongozi waliotoa mchango mkubwa katika kumaliza mgomo wa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Amesema mgomo huo, ambao ulisababisha chuo kufungwa kwa muda, ulihitaji uchunguzi wa kina na mapendekezo madhubuti ili kutafuta suluhisho. 

Kwa mujibu wa Warioba, Prof. Sarungi alipewa jukumu hilo na alitoa mapendekezo yaliyosaidia kumaliza mgogoro huo kwa mafanikio.